Posts

Showing posts from June, 2024

DK MOLLEL AWASHUKIA WATUMISHI WA UMMA WANAOFUNGIA VITUO VYA KULELEA WATOTO

Image
Muhtasari: Maofisa ustawi wa jamii wametakiwa kuacha tabia ya kuvifungia vituo vya kulelea watoto wanaoishi  kwenye mazingira magumu na hatarishi bila kuwa na mbadala wa mahali pa kuwapeleka watoto hao. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. NAIBU Waziri wa afya, Dk Godwin Mollel amewataka watumishi wa umma kuacha kuvifungia vituo vya kulelea watoto bila kujua watawapeleka wapi watoto hao baada ya vituo hivyo kufungwa. Dk Mollel ametoa kauli hiyo leo alhamisi Juni 27, 2024 wakati akizungumza  kwenye mkutano Mkuu wa kituo cha kulelea watoto wanaloishi kwenye mazingira magumu na hatarishi Kisedet  kilichopo Kata ya Chigongwe Jijini Dodoma. Dk Mollel amesema kitendo hicho kinawakatisha tamaa watu ambao wamejitolea kuwalea watoto katika mazingira waliyonayo hivyo badala ya kuvifungia vituo hivyo wanatakiwa waviboreshe ili watoto wasizagae hovyo  mitaani. "Unakuta mtu ameamua kuwakusanya na kuwalea watoto baada ya kuwaokota huko mitaani anakuja mtumishi wa umma anakifunga hicho kituo...

TLS: SHERIA YA UHURU WA KUJIELEZA IENDANE NA MABADILIKO YA SAYANSI NA TEKNOLOJIA

Image
Muhtasari: Chama cha wanasheria wa Tanganyika (TLS) kimesema ili sheria ya uhuru wa kujieleza ifanye kazi vizuri kama ilivyoelezwa kwenye kifungu cha katiba namba 18 ni lazima katiba ifanyiwe marekebisho upya ili kifungu hicho kiendane na mabadiliko ya sayansi na teknolojia yaliyopo hivi sasa ambayo yanaafanya baadhi ya mipaka  ya kujieleza iliyopo kwenye katiba kushindwa kutekelezeka. Na Mwandishi Wetu, Dodoma  MAKAMU wa Rais wa Chama cha wanasheria wa Tanganyika (TLS) Deus Nyabiri amesema upo ulazima wa kuifanyia marekebisho katiba ya nchi ili iendane na sayansi na teknolojia ya sasa hasa kwenye kifungu cha uhuru wa kujieleza. Nyabiri ametoa wito huo leo jumanne Juni 25, 2024 wakati akifungua mafunzo ya kuwajengea uwezo  mawakili kuhusu uhuru wa kujieleza Jijini Dodoma. Mwanasheria huyo mwandamizi amesema kila mtu Duniani ana uhuru wa kujieleza tangu anapozaliwa na hata katiba ya nchi imelieleza hilo lakini kwa sasa kutokana na mabadiliko ya sayansi na teknolojia kuna h...

WATU WENYE UALBINO WALIA NA WAGANGA WA KIENYEJI NA UCHAGUZI MKUU

Image
 Muhtasari: Waganga wa kienyeji na suala la uchaguzi mkuu vimetajwa kuwa haviwezi kukwepa lawama za ukatili na mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) kwani kila kinapofika kipindi cha uchaguzi ndipo ukatili huo hutokea na waganga wa kienyeji wakitajwa kuwa ndiyo chanzo cha ukatili huo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma Taasisi ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) ya Foundation for disabilities hope (FDH) imesema kuwa waganga wa kienyeji na suala la uchaguzi mkuu hawawezi kukwepa lawama za ukatili wa watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) kwani kila yanapotokea mauaji ya watu hao ni lazima watajwe. kauli hiyo imetolewa Leo jumatatu Juni 24, 2024 na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo, Michael Salali wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matukio ya kujeruhiwa na kuuawa kwa watu wenye ualbino nchini Jijini Dodoma. Salali amesema Taasisi hiyo inalaani tukio la kujeruhiwa kwa mtoto Julius Kazungu (10) mkazi wa Mkoani Geita na watu wasiojulikana pamoja na kutekwa na kisha kuuawa kwa m...

WACHIMBAJI WADOGO WATAKIWA KUTUMIA TEKNOLOJIA ZA KISASA KUCHENJUA MADINI BADALA YA KUTUMIA KEMIKALI YA ZEBAKI

Image
  Muhtasari: Wachimbaji wadogo wa madini nchini   wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya kemikali ya zebaki inayotumika kwenye uchenjuaji wa madini ili kulinda afya zao na madhara yatokanayo na matumizi mabaya ya kemikali hiyo ikiwemo magonjwa ya ngozi, figo, kifua na hata kifo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WACHIMBAJI wadogo wa madini nchini wametakiwa kuzingatia matumizi sahihi ya kemikali ya zebaki inayotumika kuchenjulia madini ili wajiepushe na madhara yanayotokana na matumizi holela ya kemikali hiyo ikiwemo magonjwa ya ngozi, figo, saratani, kifua na hata kifo. Ushauri huo umetolewa leo jumamosi Juni 22, 2024 na Baraza la Taifa la usimamizi wa mazingira (NEMC) na Ofisi ya   Mamlaka ya maabara ya mkemia mkuu wa serikali wakati wakitoa semina ya matumizi sahihi ya kemikali ya zebaki kwa wachimbaji wadogo wa madini nchini waliokutana Jijini Dodoma. Akizungumza kwenye mafunzo hayo Mratibu wa Mradi wa Kudhibiti Matumizi ya Zebaki kwa Wachimbaji Wadogo  (...

WATOTO WAPAZA SAUTI KUHUSU KUFANYIWA VITENDO VYA UKATILI

Image
Muhtasari: Kwa mujibu wa takwimu za Wilaya cha Chamwino za Oktoba 2023 hadi Juni 2024 kesi za ukatili zilizoripotiwa kituo cha polisi  Chamwino zilikuwa 118 kati ya hizo wanaume 109, wanawake 9, watoto 26, kesi 88  zipo mahakamani, 32 wameshawatiwa hatiani kwa matukio ya ubakaji, ukeketaji  na vipigo. Na Mwandishi Wetu, Chamwino BARAZA la ulinzi wa mtoto wilaya ya Chamwino Mkoani Dodoma limeitaka  serikali kushirikiana na wadau mbalimbali kuboresha sera na sheria ya ulinzi wa watoto ikiwamo sheria ya ndoa yam waka 1971 inayoruhusu mtoto mwenye umri wa miaka 14 kuolewa ili kutokomeza ukatili  dhidi yao. Wito huo umetolea leo Ijumaa Juni 21, 2024  na mwenyekiti wa Baraza hilo Anthony Mlewa wakati wa  kilele cha maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika  yaliofanyika katika Kijiji cha Kawawa kata ya Msanga wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma yaliyoandaliwa na shirika lisilo la kiserikali la Actionaid  Tanzania yenye kauli mbiu; elimu jumuishi kwa wato...

VITA DHIDI YA VIMELEA SUGU VYA DAWA YATINGA BUNGENI

Image
 Muhtasari: Wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. wamezindua umoja wao wa kukabiliana na usugu wa vimelea vya dawa (uvida) nchini ambapo wameahidi kutunga sheria na sera zitakazomaliza tatizo hilo nchini ambalo linakuwa kwa Kasi. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WABUNGE wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambao ni vinara wa kupinga usugu wa vimelea vya dawa (uvida) wamesema kuwa watasimamia utungwaji wa sera na sheria nchini zitakazowezesha kumaliza tatizo hilo ambalo limetajwa na Shirika la afya Duniani kama janga linaloikabili jamii kwa sasa. Kauli hiyo imetolewa leo alhamisi Juni 20, 2024 na Mwenyekiti wa umoja huo Dkt Hamis Kigwangala wakati wa uzinduzi wa umoja huo uliofanywa na Shirika la One Healthy Society Jijini Dodoma. Dkt Kigwangala amesema imefika wakati sasa wa kutunga sheria na sera zitakazomaliza tatizo hilo la usugu wa vimelea vya  dawa kwani likiachwa likaendelea litasababisha madhara makubwa ikiwemo vifo na kuporomoka kwa uchumi. Mwenyekiti w...

VIUNGO KWA BINADAMU HAVIHUSIANI NA TIBA ASILI... WAGANGA WA TIBA ASILI

Image
 Muhtasari: Umoja wa waganga na wakunga wa tiba asili Tanzania (Uwawata) wamelaani vitendo vinavyofanywa na matapeli anaojiita waganga wa kienyeji kuwaua watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) na kusema kuwa hakuna tiba ya asili inayohusisha viungo vya binadamu. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. UMOJA wa waganga na wakunga wa tiba asili Tanzania (Uwawata) umesema kuwa hakuna tiba asili ambayo inahusisha viungo vya binadamu na kwamba wote wanaofanya vitendo hivyo ni matapeli wanatakiwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria. Kauli hiyo imetolewa leo alhamisi 20, 2024 na Katibu Mkuu wa Uwawata Taifa Lucas Mlipu wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu waganga wa kienyeji kuhusishwa na matukio ya mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albino) hasa kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa na uchaguzi mkuu wa mwaka 2025. Katibu wa umoja wa waganga na wakunga wa tiba za asili Tanzania (Uwawata) Mkoa wa Kagera, Patian Kashubi (aliyesimama) akizungumza na waandishi wa habari kula...

TISA MBARONI KWA MAUAJI YA MTOTO MWENYE UALBINO MKOANI KAGERA

Image
 

TMDA YATOA MSAADA WA DAWA NA VIFAA TIBA VYENYE THAMANI YA SH 24 MILIONI

Image
  Muhtasari: Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) Kanda ya kati imetoa msaada wa vifaa tiba, dawa na vitendanishi vyenye thamani ya Sh24 milion kwenye gereza kuu la Isanga lililoko Mkoani Dodoma kwa ajili ya kuwahudumia wafungwa, mahabusu na askari magereza wapatao 1,489. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAMILIKI wa maduka ya dawa nchini wametakiwa kufuata masharti ya leseni zao za kufanya biashara hiyo ili wasihatarishe afya za watumiaji. Kauli hiyo imetolewa leo jumanne Juni 18, 2024 na Meneja wa Mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) kanda ya kati, Sonia Mkumbwa wakati akitoa msaada wa dawa, vifaa tiba na vitendanishi vyenye thamani ya Sh24 milion kwenye gereza kuu la Isanga lililopo Mkoani Dodoma. Mkumbwa amesema dawa hizo zimepatikana kwenye msako unaofanywa na mamlaka hiyo kwenye maduka ya dawa na vitendanishi ambavyo vimekuwa vikihifadhiwa kwenye maeneo ambayo hayapaswi kuhifadhiwa. Meneja wa mamlaka ya dawa na vifaa tiba (TMDA) Kanda ya kati, Sonia Mkumbwa (wa tano kulia) a...

MWANDISHI WA HABARI MATHIAS CANAL ACHANGIA SH MIL 1 KWA AJILI YA MADAWATI

Image
 Mutasari: Shule ya msingi  Kigasha  imejengwa kwa nguvu ya wananchi wa jimbo hilo ambao wamejenga madarasa mawili na Mbunge wake Innocent Bashungwa alichangia mabati kwa ajili ya kupaua Na Mwandishi Wetu, Karagwe KUFUATIA juhudi zinazofanywa na Mbunge wa Jimbo la Karagwe Innocent Bashungwa katika kuimarisha sekta ya elimu ikiwemo ujenzi wa shule mpya ya msingi ya Kigasha, Mwandishi wa habari nchini  Mathias Canal amechangia kiasi cha Shilingi Milioni 1 kwa ajili ya madawati. Mathias amechangia madawati hayo mara baada ya kutembelea shule hiyo iliyopo katika kata ya Rugu, Tarafa ya Nyaishozi Wilayani karagwe Mkoani Kagera akiwa katika kazi ya kutembelea miradi ya maendeleo ikiwa ni sehemu ya kujionea utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2020/2025.                                                       Mwandis...

WAISLAM WATAKIWA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Image
 Muhtasari: Waumini wa dini ya kiislamu wametakiwa kujitokeza kwa wiingi kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa ili waweze kuhoji au kupongeza yale yanayoendelea nchini. Na Mwandishi wetu, Dodoma. Dodoma. Waumini wa dini ya kiislamu nchini wametakiwa kujitokeza kwa wingi na kushiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa kulingana na ratiba itakayotolewa na serikali. Kauli hiyo imetolewa leo jumatatu Juni 17, 2024 na mwakilishi wa mufti wa Tanzania, Shekhe Swedi Twaibu kwenye ibada ya swala ya Eid El Adha iliyofanyika kwenye uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma. Shekhe Twaibu amesema ni jukumu la waumini wa dini hiyo kushiriki kila jambo ambalo kinaendelea nchini ili wawe nafasi ya kuhoji au kupongeza yale yanayoendelea nchini. "Mufti wa Tanzania (Shekhe Aboubakar Zubeir) amenituma kwenu niwaambie kuwa mshiriki kwenye uchaguzi wa serikali za mitaa msiliache jambo hili liwapite mjitokeze kwa wingi kuwachagua viongozi watakaowaongoza kwa misingi ya haki," amesema Shekhe Twaibu. Pia ame...

DAFTARI LA WAPIGA KURA HALIHUSIKI NA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Image
 Muhtasari: Mkutano huo unahitimisha mfululizo wa mikutano ambayo Tume imefanya na wadau wake kuanzia Juni 7 mwaka huu ambapo baadae tume hiyo itafanya mikutano ya kutoa elimu na wadau kwenye mikoa yote kwa kuzingatia ratiba ya uboreshaji wa Daftari la kudumu la wapiga kura Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam UBORESHWAJI wa Daftari la Kudumu la Wapiga Kura hauhusiani na maandalizi ya uchaguzi wa serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika mwaka huu wa 2024.  Hayo yamesemwa na Mkurugenzi wa Uchaguzi wa Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ramadhani Kailima, wakati akifungua mkutano wa Tume na Maafisa Habari wa Mikoa na Halmashauri Leo jumamosi Juni 15, 2024 jijini Dar es Salaam.  Mkutano huo unahitimisha mfululizo wa mikutano ambayo Tume imefanya na wadau wake kuanzia  Juni 7 mwaka huu ambapo  baadae Tume hiyo itafanya mikutano na wadau kwenye mikoa yote kwa kuzingatia ratiba ya uboreshaji wa Daftari. Mikutano hiyo ina lengo la kuwapa wadau taarifa za uwepo wa zoezi la ubor...

Kituo cha kwanza cha taarifa za mapema za majanga Barani Afrika kimezinduliwa Tanzania

Image
 Muhtasari: Serikali imezindua chumba cha taarifa za tahadhari za mapema za majanga ambacho kitaiwezesha serikali kuchukua hatua mapema za majanga kabla hayajatokea nchini. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Bunge Sera na Uratibu, Jenista Mhagama amezindua chumba cha taarifa za tahadhari ya mapema kuhusu majanga nchini kitakachowezesha serikali kuchukua hatua za haraka kabla majanga hayo hayajatokea. Kituo hicho ambacho ni cha kwanza kujengwa Barani Afrika kimezinduliwa leo ijumaa Julai 14, 2024 Jijini Dodoma ambapo kimejengwa kwa ufadhili wa Shirika la maendeleo la nchini Italia (AICS) ambacho kitakuwa na mfumo utakaowezesha kufuatilia, kuchambua na kuratibu taarifa na takwimu za majanga, hali ya uwezekano wa kuathirika, utabiri wa hali ya hewa na haidrolojia hatarishi na uchambuzi wa madhara yanayoweza kutokea. Mhagama amesema chumba hicho kitasaidia serikali kuchukua hatua za haraka kwa ajili ya kukabiliana na majanga ya mvua kubwa za el nino, mafuri...

BODI YA TAWA KUJA NA MIKAKATI KABAMBE YA KUIBORESHA HIFADHI YA PANDE

Image
Muhtasari: Mojawapo ya mikakati hiyo ni kuwatumia wasanii wa Bongo Movie kutangaza hifadhi hiyo pamoja na kuanzisha bustani za wanyama hai ambao watakuwa kivutio kwa watalii wa ndani watakaokwenda kupumzika kwenye hifadhi hiyo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyapori (TAWA) Meja Jenerali Mstaafu, Hamis Semfuko amesema Bodi anayoiongoza imejipanga kuja na mipango madhubuti ya kuifanya Hifadhi ya Pande iliyopo Jijini Dar es Salaam kuwa kivutio kikubwa kwa watu waishio  ndani na nje ya Jiji hilo. Akizungumza na waandishi wa habari    katika ziara  iliyofanyika jana Juni 13, 2024 hifadhini humo, Semfuko amesema  Bodi yake imedhamiria kuwafanya watanzania waione Hifadhi ya Pande kuwa ni sehemu ya kipekee kwa ajili ya kustarehe na kupumzisha akili zao, na kwa kuanzia imeanzisha bustani wa wanyamapori hai ndani ya hifadhi hiyo ambao wako huru kutembea "free roaming" ikiwa na wanyamapori mbalimbali kama vile nyum...

NGOs ZAPEWA MWONGOZO WA KULIPA KODI NA TRA

Image
 Muhtasari: Mamlaka ya mapato nchini (TRA) imezindua kitabu cha mwongozo wa kulipa kodi kwa asasi za kiraia zinazotokana na fedha wazopata kwa ajili ya miradi mbalimbali inayotekelezwa nchini Na Mwandishi Wetu, Dodoma Ili kupunguza malalamiko ya kodi zinazokatwa kwenye fedha za miradi inayotekelezwa na asasi za kiraia nchini (NGOs) mamlaka ya mapato nchini (TRA) imezindua kitabu cha mwongozo wa kulipa kodi kwa asasi hizo. Kitabu hicho kimezinduliwa  na Kamishna wa kodi za ndani, Alfred Mregi kwa kushirikiana na mtandao wa utetezi wa haki za binadamu (THRDC) Jijini Dodoma. Akizungumza kwenye uzinduzi huo Mkurugenzi wa THRDC, Onesmo Olengurumwa amesema bado kuna faini na riba ambazo huwa zinatozwa na TRA hata kama asasi inakuwa haina mradi unaotekelezwa kwa sababu tu imeshaingizwa kwenye mfumo wa kulipa kodi. Amesema hiyo huwa inasababisha asasi kuwa na madeni makubwa ya kodi pale wanapopata miradi kwani huwa inaonyesha kuwa hawalipi kodi wakati kodi zao huwa zinatokana na fedha...

WASOMI WA UDOM WATWISHWA JUKUMU LA KUBORESHA MAZINGIRA YA JIJI LA DODOMA

Muhtasari: Wasomi wa chuo kikuu cha Dodoma (Udom) wametakiwa kurejesha uoto wa asili wa Jiji la Dodoma kwa kuanzisha vitalu vya miti ya asili na kuipanda kwenye maeneo ambayo yana uharibifu mkubwa wa mazingira. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WANAFUNZI wanaosoma chuo kikuu cha Dodoma (Udom) wametakiwa kuanzisha kitalu cha miti ya asili ambayo itapandwa kwenye maeneo yenye uharibifu mkubwa wa mazingira Jijini Dodoma ambao utakuwa mchango wa uwepo wa chuo hicho Jijini humo. Kauli hiyo imetolewa  na Makamu Mkuu wa Chuo hicho Profesa Lughano Kusiluka kwenye mdahalo wa maadhimisho ya siku ya mazingira duniani uliofanyika chuoni hapo na kuwashirikisha wataalam na wanafunzi wa idara ya mazingira. Profesa Kusiluka amesema chuo hicho kina wataalam mbali wa masuala ya mazingira hivyo watumie utaalam wao kuhakikisha kuwa Jiji la Dodoma linarejesha uoto wake wa asili ambao umepotea na kusababisha ukame. “Hii elimu mnayoitoa hapa chuoni tuione ikifanya kazi kwenye mazingira ya nje ya chuo ili tujue ...

Ndoa za utotoni zinazima ndoto za wasichana

Image
Muhtasari: Shirika lisilo la kiserikali la Msichana Initiative limeitaka serikali kuharakisha muswada wa mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kwani imekuwa chanzo cha wasichana wengi kuolewa ndoa za utotoni chini ya miaka 18 na wazazi kujificha kwenye kichaka cha sheria hiyo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. SHIRIKA lisilo la kiserikali la Msichana Initiative ambalo linajishughulisha na mapambano ya ukatili dhidi ya wasichana nchini limeitaka serikali kuharakisha muswada wa mabadiliko ya sheria ya ndoa ya mwaka 1971 kwani imekuwa chanzo cha wasichana wengi kuolewa ndoa za utotoni chini ya miaka 18 na wazazi kujificha kwenye kichaka cha sheria hiyo. Akizungumza kwenye mkutano wa kitaifa majukwaa ya wanajamii Jijini Dodoma, Mkurugenzi Mtendaji wa shirika hilo, Rebeca Gyumi amesema shirtika  la msichana Initiative limekuwa ni moja ya mashirika vinara nchini kupambania mabadiliko ya sheria ya ndoa.  Amesema kutokana na mkanganyiko wa umri wa kuolewa mtoto wa kike  shirika hil...