TSC YAKABIDHIWA MAGARI KWA AJILI YA KUTEMBELEA WALIMU NA KUJUA CHANGAMOTO ZAO
Muhtasari: Tume ya utumishi wa walimu imetakiwa kutatua changamoto na kero za walimu nchini na kama kuna wenye changamoto za kisaikolojia watafutiwe huduma ya ushauri nasaha ili wawasaidie utekeleza majukumu yao ya kutoa elimu wa Watanzania. Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), Mohamed Mchengerwa ameiagiza tume ya utumishi wa walimu (TSC) kughulikia kero na changamoto za walimu nchini ili kuondoa malalamiko yote ya walimu na kama kuna walimu watakuwa na changamoto za kisaikolojia wawape huduma ya ushauri nasaha. Mchengerwa ameyasema hayo leo jumapili Agosti 11, 2024 wakati akikabidhi magari 10 kwa makatibu wasaidizi wa wilaya wa tume ya utumishi wa walimu jijini Dodoma na kuwataka kuyatumia magari hayo kuwatembelea walimu kwenye vituo vyao vya kazi ili kujua changamoto walizonazo badala ya kukaa maofisini na kusubiri walimu wawafuate. Sehemu ya magari 10 ambayo yamewagawiwa kwa makatibu wasaidizi wa Wilaya wa tume ...