Posts

Showing posts from July, 2024

ESWATIN YAJA KUJIFUNZA NAMNA YA KUENDESHA MIFUKO YA HIFADHI ZA JAMII PSSSF

Image
Muhtasari: Ujumbe wa watu tisa kutoka nchini Eswatin wametembelea mfuko wa hifadhi ya jamii wa PSSSF ili kujifunza namna bora ya uendeshaji wa mifuko ya pensheni na kuachana na mfuko wa akiba ambao bado unatumika nchini humo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma SERIKALI imesema kuwa itapeleka wataalam wa kuendesha mifuko ya hifadhi za jamii kutoka mfuko wa PSSSF nchini Eswatin ili kuwafundisha namna kuanzisha mfuko wa hifadhi ya jamii unaotoa pensheni kwa wanachama wake na kuachana na mfuko wa akiba ambao unatumika nchini humo kwa sasa. Hayo yamesema leo ijumaa Julai 19, 2024 na Mkurugenzi Mkuu wa mfuko wa hifadhi ya jamii wa PSSSF Abdul-Razaq Badru baada ya kupokea ujumbe wa viongozi tisa akiwemo waziri wa utumishi wa umma kutoka nchini Eswatin kwa ajili ya ziara ya kuja kujifunza uendeshaji wa mifuko ya hifadhi ya jamii inayotoa pensheni kwa wanachama wake. Badru amesema nchi ya Eswatin bado inatumia mfuko wa akiba kwa wanachama wake na wanataka kuanza kutoa pensheni hivyo wamekuja kujifunza n...

KUTOKA KUOMBA OMBA HADI KUMILIKI DUKA LAKE

Image
Muhtasari: Mwanamke huyo ambaye ni mlemavu wa viungo kwa sasa anamiliki duka ambalo limemsaidia kuachana na kuomba msaada kwa watu na sasa anaihudumia familia yake ya watu wanne kutokana na biashara hiyo ya duka. Na Mwandishi Wetu, Chamwino. MKAZI wa Kijiji cha Majeleko kilichopo Wilayani Chamwino Mkoani Dodoma, Melea Obed ambaye ni mlemavu wa viungo amejikuta akiachana na kazi ya kuomba misaada kwa watu baada ya kupata ufadhili wa kufunguliwa duka la kuuza mahitaji ya nyumbani. Akizungumza na Kirimbo Blog leo jumatano, Julai 2024 Melea ambaye hawezi kukaa wala kutembea kutokana na ulemavu alionao amesema kabla ya kufunguliwa biashara ya duka alikuwa anashinda ndani  hata miezi minne bila kutoka nje. Picha ikionyesha duka lililojengwa na mbao ambalo linamilikiwa na mlemavu wa viungo Melea Obed aliyekaa kwenye kiti mwendo.. Anayemwendesha ni Latwifa Saninga kutoka Shirika la Brac Maendeleo Amesema hiyo inatokana na kutokuwa na uwezo wa kufanya shughuli yoyote kwa kuwa hawezi...

KIHENZILE AAGIZA UWANJA WA NDEGE WA KIMATAIFA MSALATO UKAMILIKE KWA WAKATI

Image
Muhtasari: Mkandarasi anayejenga uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Msalato ametakiwa kuongeza kasi ya ujenzi wa uwanja huo ili ukamilike kwa wakati kwani ni mojawapo ya alama za kuonyesha kuwa Dodoma ni makao makuu ya nchi. Na Mwandishi Wetu, Dodoma NAIBU waziri wa Uchukuzi, David Kihenzile ameagiza mkandarasi anayejenga uwanja wa ndege wa kimataifa wa Msalato uliopo Jijini Dodoma kukamilisha ujenzi huo  kwa wakati kwani ni mojawapo ya alama zinazoonyesha kuwa Dodoma ni makao makuu ya nchi. Kihenzile ametoa kauli hiyo leo alhamisi Julai 11, 2024 alipofanya ziara ya kukagua ujenzi wa uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Msalato uliopo Jijini Dodoma. Sehemu ya ujenzi wa majengo ya uwanja wa ndege wa kimataifa wa Msalato uliopo Jijini Dodoma Amesema uwanja huo ni lango la utalii kwenye hifadhi mbalimbali za taifa ikiwemo Serengeti, Ruaha na maeneo mengine ya utalii kwa kuwa ni rahisi kufika kwenye maeneo hayo kutokea Dodoma. “Mbali na reli ya mwendo kasi inayopita hapa, lakini pia uwanja huu...

KATIBU MKUU CCT: VIJANA SIMAMIENI MIRADI YA MAENDELEO KWENYE MAENEO YENU

Image
Muhtasari: Vijana nchini wametakiwa kufuatilia miradi ya maendeleo iliyopo kwenye maeneo yao kwa sababu inajengwa kwa kutumia kodi zao hivyo kama inajengwa kwa kusuasua au chini ya kiwango ni lazima wachukue hatua za kuwawajibisha waliowapa dhamana ya kusimamia miradi hiyo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma KATIBU Mkuu wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT) Dk Moses Matonya amewataka wananchi kukagua miradi inayotekelezwa kwenye maeneo yao ili kujua kama inatekelezwa kwa ubora na kiwango kinachotakiwa kwa sababu inajengwa kwa kutumia kodi zao. Dk Matonya ametoa kauli hiyo leo jumatano julai 10, 2024 wakati akizungumza na vijana kwenye semina iliyotolewa na taasisi isiyo ya kiserikali ya mtandao wa madeni na maendeleo (TCDD) Jijini Dodoma. Amesema serikali inatekeleza miradi mingi kuanzia ngazi ya vijiji, kata, Halmashauri hadi serikali kuu lakini vijana hawaijui miradi hiyo wala utekelezaji wake kwa sababu wanadhani ni mambo ambayo hayawahusu, na kuwataka kufuatilia miradi hiyo kwa sababu ni ko...

CHODAWU YAITAKA SERIKALI KURIDHIA MKATABA NAMBA 189 WA WAFANYAKAZI WA MAJUMBANI

Image
Muhtasari: Wafanyakazi wa majumbani wameitaka serikali kuridhia  mkataba namba 189 wa Shirika la kazi Duniani (ILO) ili kada hiyo iweze kutambulika kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine nchini. Na Mwandishi Wetu, Dodoma WAFANYAKAZI wa majumbani wameiomba serikali kuridhia mkataba namba 189 wa Shirika la kazi Duniani (ILO) kuhusu  kazi za staha kwa wafanyakazi wa majumbani ili waweze kupata haki zao kama wafanyakazi wengine ikiwemo likizo, kujiunga na mifuko ya hifadhi za jamii na kulipwa kima cha chini cha mshahara. Kauli hiyo imetolewa leo jumanne na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Light for Domestic Workers (LDW) ambayo inajishughulisha na kutoa elimu kuhusu wafanyakazi wa majumbani kujua haki na majukumu yao, Beatrice Johnson wakati akizungumza kwenye mkutano mkuu wa chama cha wafanyakazi wa mahotelini na majumbani (Chodawu) Jijini Dodoma. Beatrice amesema wafanyakazi wa majumbani wanapitia changamoto nyingi kwenye maeneo yao ya kazi kwa kuwa hakuna sheria inayowalinda kwan...

MWONGOZO WA KUVUA SAMAKI KWENYE MAJI MADOGO WATOLEWA

Image
Muhtasari: Wizara ya mifugo na uvuvi kwa kushirikiana na mamlaka za serikali za mitaa, ofisi ya Rais Mipango na uwekezaji na Ofisi ya makamu wa Rais Mazingira zimetakiwa kutoa elimu kuhusu uvuvi endelevu kwenye maji madogo na maeneo oevu ili kulinda na kutunza rasilimali hiyo ambayo imeajiri watu wengi nchini. Na Mwandishi Wetu, Dodoma. WADAU wa uvuvi nchini wametakiwa kutoa elimu ya uvuvi endelevu kwa wavuvi wanaofanya shughuli zao kwenye maji madogo na maeneo oevu nchini ili kufanya uvuvi huo uwe endelevu na wao waendelee kujipatia kipato bila kuvunja sheria na miongozo iliyopo. Kauli hiyo imetolewa leo ijumaa jUNI 28, 2024 na Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dk Edwin Mhede wakati akizungumza na wadau wa uvuvi kwenye kikao cha kupitia rasimu ya mwongozo wa usimamizi wa uvuvi kwenye maji madogo na maeneo oevu Jijini Dodoma. Dk Mhede amesema wavuvi wengi hawajui sheria na miongozo kuhusu uvuvi kwenye maji madogo na maeneo oevu  inavyotumika hivyo ni wajibu wa Wizara y...

PBZ YATOA MSAADA WA JOKOFU LA KUHIFADHIA DAMU

Image
Muhtasari: Msaada huo utawezesha kuanzishwa kwa huduma ya mama na mtoto pamoja na upasuaji kwa akina mama wanaojifungua katika kituo hicho cha afya ambacho hakijaanza kutoa huduma ya kujifungua kutokana na kutokuwa na jokofu la kuhifadhia damu  Na Mwandishi Wetu, Dodoma. KITUO cha afya kilicho chini ya jeshi la polisi mkoa wa Dodoma kitaanza kutoa huduma ya mama na mtoto kuanzia Agost 1, mwaka huu baada ya kukamilisha mahitaji yote yanayotakiwa katika wodi hiyo ikiwemo jokofu la kuhifadhia damu kwa wenye uhitaji. Kauli hiyo imetolewa leo jumatatu Julai 1, 2024 na mganga mfawidhi wa kituo hicho Dk Jackson Shoo wakati akipokea msaada wa jokofu la kuhifadhia damu lenye uwezo wa kuhifadhi lita 360 kwa wakati mmoja kutoka Benki ya Watu wa Zanzibar (PBZ) Jijini Dodoma. Jokofu la kuhifadhia damu lililotolewa na benki ya watu wa Zanzibar (PBZ) likiwa kwenye wodi ya wazazi  inayotarajiwa kuanza kazi Agosti 1 mwaka huu baada ya kukamilisha mahitaji yote muhimu kwenye kituo cha afya cha ...