POLISI DODOMA KUKABILIANA NA VITENDO VYA UHALIFU
Muhtasari: Kutokana na kushamiri kwa matukio ya ukatili Mkoani Dodoma dawati la jinsia na watoto la polisi limekuja na kampeni kabambe ya kupunguza vitendo vya ukatili wa kijinsia na watoto mkoani humo. Na Mwandishi Wetu, Dodoma DAWATI la jinsia na watoto la polisi mkoa wa Dodoma limekutana kwenye kikao kazi maalum cha kujadili matukio ya ukatili yanayoendelea mkoani humo ili kujua namna ya kukabiliana nayo. Mkuu wa dawati la jinsia Mkoa wa Dodoma ambaye pia ni mrakibu msaidizi wa jeshi la polisi Christer Kayombo ameyasema hayo leo alhamisi Septemba 17, 2024 kwenye kikao kazi kilichowakutanisha wadau mbalimbali wa kupinga ukatili wa kijinsia na watoto Jijini Dodoma. Christer amesema wameamua kutoa mafunzo hayo kwa polisi wa dawati la jinsia na watoto kwa lengo la kuwawezesha kuondoa matukio ya ukatili ambayo yameshamiri katika mkoa wa Dodoma. “Sisi kama mkoa tuliona ipo haja ya kufanya kitu cha ziada ili kupambana na matendo ya ukatili, tukaamua kuandaa mafunzo h...